RSS Feed

Tag Archives: Zanzibar

Habari ya jana 1: Profesa Safari ajiunga na CHADEMA

Posted on

Nilipozisikia habari za mtu ninayempenda na kumheshimu kama mwanataaluma na mwanafalsafa mzuri kati ya wanazuoni wa Tanzania, Prof. Safari kwamba amejiunga na kambi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akitokea Chama cha Wananchi (CUF) sikushangaa sana.

Kwanza, CUF kwa siku za karibuni wamekosa ile kasi yao na ‘upinzani’ wa kweli. Matamshi ambayo amekuwa akiyatoa mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibarahim Lipumba, yamekuwa yakionyesha dhahiri kwamba CUF ile tuliyoijua imebadilika na sasa imekuwa kama ‘CCM (b)’. Siwezi kuwalaumu sana CUF kwa mabadiliko hayo, nafikiri walikosea pale ambapo walishindwa kubashiri madhara ya muafaka kati yao na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa upande wa Zanzibar. Wakajikuta kwenye mtego ambao na kuingia na sasa wanalipa gharama. Kwa hiyo kwa mtu yeyote ndani ya CUF ambaye angependa kushindana na siasa za CCM hana jinsi bali kutafuta uwanja mwingine.

Pili, na hii ni kama ushauri kwa uongozi wa CHADEMA. Inawezekana (mimi sina uhakika) aliye-injinia ‘muafaka’ kati ya CCM na CUF ni huyo huyo mliyepokea jana. Kwa hiyo muwe macho nyie CHADEMA isije ikawa ujio wa Safari umeandaliwa makusudi ili kupunguza makali yenu. Msiwe na haraka ya kumpa uongozi hadi hapo mtakapohakikisha kwamba huyo mtu hana ajenda ya siri. Ni tahadhari tu wala sina ‘bifu’ yoyote na profesa.

Aliyosema Kikwete

Posted on

Masuala ya walimu

Nyaraka, Ilani na miongozo (vilivyotolewa na viongozi wa dini)

Yaliyojiri kwenye kikao cha NEC-CCM, Dodoma

Ufisadi, rushwa na mafisadi

Kesi ya Zombe

Nimeomba pesa, nimeomba pesa, nimeomba pesa — ADB, Benki ya Dunia, Serikali ya Saudi Arabia, Serikali ya China
(alikuwa akirudia-rudia)

Miundombinu: Lindi, Mtwara, Kigoma, Kagera

Suala la Richmond *kampuni kanyaboya*. Kumbe hata yeye aliishutukia.

Uhuru wa vyombo vya habari

Masuala ya Muungano na Zanzibar

Falsafa ya maisha bora kwa kila mtanzania

Ambayo hakuyasema:

  • Tatizo la mtikisiko wa uchumi duniani
  • Ukame na njaa katika mikoa ya kaskazini

Observations:

Tido Mhando tunayemjua sio yule mwandishi wa habari machachari wa BBC aliyekuwa na maswali ya kichokozi. That tells you something: If you are not careful, you will be changed by the system instead of you changing it.

Access to clean water in rural areas of Tanzania is still a problem

Access to clean water in rural areas of Tanzania is still a problem

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.