Tag Archives: watoto
Usafiri wa umma (mijini) Tanzania

City public transport in Tanzania is not suitable for children, the elderly and disabled
Leo wakati nakuja kazini nilitumia usafiri wa daladala. Pale nilikopandia daladala kulikuwa na akina mama ambao umri wao ulikuwa umeenda kidogo. Kwa kweli niliwahurumia. Hakuna jinsi ambavyo unaweza kupanda daladala bila kusukumana. Na kwa umri wa hao mama zangu nilikuwa na wasiwasi kwamba kwa kweli ingewawia ngumu kupata usafiri.
Ukijaribu kuangalia usafiri wetu wa umma hasa ule wa mijini utakubaliana na mimi kwamba si usafiri ambao watoto, wazee na wenye ulemavu wanaweza kuutumia bila matatizo.
Si wazee wengi wanaoweza kupanda gari kwa kupitia dirishani. Si watoto wengi wanaweza kusukumana ili kupenya kwenye mlango na kuingia ndani ya basi. Wala si walemavu wengi wanaoweza kubanana kwenye gari ili waweze kufika waendako.
Hili ni tatizo la kiuongozi kwani kuwa na usafiri wa kistarabu mijini inawezekana. Inaweza kufanyika kirahisi zaidi kuliko KILIMO KWANZA.


