
Wakati umefika wa kuwa na katiba inayo-cover changamoto tunazokumbana nazo leo
Matatizo na changamoto kadhaa tunazokutana nazo leo zinahitaji kuwa na sheria-mama inayoweza kupambana nazo. Kuna mambo mengi yanaendelea kujitokeza hapa Tanzania, hasa ya kimaadili ya uongozi na utawala bora, ambayo katiba yetu ya sasa ama haisemi au inasema kwa namna ambayo haiwezi kutufanya kuwa na viongozi wenye kuzingatia maadili na misingi ya utawala bora.
Tuchukulie mfano mmoja ambao mimi binafsi unanichefua sana. Watu wanatuhumiwa kwa ufujaji/wizi wa mali/pesa za nchi lakini bado unaona wamekaa bungeni.
Jamaa hao hao wanaohusishwa na wizi wa mali za nchi bado wamekaa kwenye chombo cha kutunga sheria. Hii ni hatari. Mtu leo anang’atuka/anajiuzulu kwa kashfa mbaya ya wizi wa mali za Watanzania lakini unamwona bado anachangia mijadala bungeni.
Meseji tunayotuma kwa wapiga kura wake ni hii: huyu bwana yuko safi ila sema tu tumempiga stop. Vichekesho.
Tunatakiwa kuwa na sheria inayosema hivi: kiongozi wa serikali wa ngazi yoyote anapokuwa amehusishwa kwa namna yoyote na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora atasimamishwa mara moja kufanya kazi za kiuongozi katika nchi hadi hapo vyombo husika vitakapom-declare kwamba yeye ni safi.
Naomba kuto hoja.