Wapendwa wasomaji wa blog ya viongozi. Kwanza nawapa pole sana na majukumu yenu ya siku kwa siku ya ujenzi wa Taifa letu ‘changa’ la TZ. Tusichoke.
Pili niwape hongera kwa sikukuu za Pasaka, Muungano na Mei Mosi. Naamini tumezitumia siku hizo kutafakari mambo kadhaa yahusuyo mustakabali wa Taifa letu tukufu.
Ni matumaini na maombi yangu kuwa muungano wetu ulioishi kwa mika 47 utaendelea kuwepo na kudumishwa. Naamini pia kwamba vitu vinavyotuunganisha kama Watanzania vina nguvu zaidi kuhusu kasoro tulizo nazo za muungano. Hata kama “wajinga” fulani, kwa maslahi yao binafsi, wataamua kuuvunja huu ushirikiano; bado jina Tanzania litadumu. Amin.
Sikukuu ya Mei Mosi nayo imepita — lo! Mwezi wa tano tayari!! Siku zaenda mbio kweli kweli. Sijapata nafasi ya kuyapitia yale ambayo wakuu walisema jana kwenye Mei Mosi ila naweza kusema tu kwamba TUFANYE KAZI!


