RSS Feed

Tag Archives: muungano

Tumerudi hewani tena!

Posted on

Wapendwa wasomaji wa blog ya viongozi. Kwanza nawapa pole sana na majukumu yenu ya siku kwa siku ya ujenzi wa Taifa letu ‘changa’ la TZ. Tusichoke.

Pili niwape hongera kwa sikukuu za Pasaka, Muungano na Mei Mosi. Naamini tumezitumia siku hizo kutafakari mambo kadhaa yahusuyo mustakabali wa Taifa letu tukufu.

Ni matumaini na maombi yangu kuwa muungano wetu ulioishi kwa mika 47 utaendelea kuwepo na kudumishwa. Naamini pia kwamba vitu vinavyotuunganisha kama Watanzania vina nguvu zaidi kuhusu kasoro tulizo nazo za muungano. Hata kama “wajinga” fulani, kwa maslahi yao binafsi, wataamua kuuvunja huu ushirikiano; bado jina Tanzania litadumu. Amin.

Sikukuu ya Mei Mosi nayo imepita — lo! Mwezi wa tano tayari!! Siku zaenda mbio kweli kweli. Sijapata nafasi ya kuyapitia yale ambayo wakuu walisema jana kwenye Mei Mosi ila naweza kusema tu kwamba TUFANYE KAZI!

Aliyosema Kikwete

Posted on

Masuala ya walimu

Nyaraka, Ilani na miongozo (vilivyotolewa na viongozi wa dini)

Yaliyojiri kwenye kikao cha NEC-CCM, Dodoma

Ufisadi, rushwa na mafisadi

Kesi ya Zombe

Nimeomba pesa, nimeomba pesa, nimeomba pesa — ADB, Benki ya Dunia, Serikali ya Saudi Arabia, Serikali ya China
(alikuwa akirudia-rudia)

Miundombinu: Lindi, Mtwara, Kigoma, Kagera

Suala la Richmond *kampuni kanyaboya*. Kumbe hata yeye aliishutukia.

Uhuru wa vyombo vya habari

Masuala ya Muungano na Zanzibar

Falsafa ya maisha bora kwa kila mtanzania

Ambayo hakuyasema:

  • Tatizo la mtikisiko wa uchumi duniani
  • Ukame na njaa katika mikoa ya kaskazini

Observations:

Tido Mhando tunayemjua sio yule mwandishi wa habari machachari wa BBC aliyekuwa na maswali ya kichokozi. That tells you something: If you are not careful, you will be changed by the system instead of you changing it.

Access to clean water in rural areas of Tanzania is still a problem

Access to clean water in rural areas of Tanzania is still a problem

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.