RSS Feed

Tag Archives: katiba mpya Tanzania

Kama Kiswahili ni lugha ya Taifa mbona masuala mazito ya Kitaifa yanaandikwa kwa Kiingereza?

Posted on

If, and this is constitutional, Kiswahili is our National language, why do we write matters of national concern in English? Weird!

 

Unataka kuusoma Mswada wa Katiba Mpya?

Posted on

Bonyeza hapa kusoma

Hatuhitaji kuijua Katiba ya zamani; Tunahitaji kusoma rasimu ya Katiba mpya!

Posted on

Tumefika hapa tulipo kwa sababu ya sheria-mama (katiba) tuliyo nayo sasa. Sheria mbovu, viongozi wasioweza kuwajibishwa, mamlaka makubwa aliyo nayo Rais, sheria zinazokinzana, tofauti za kisheria kati ya Zanzibar mpya na Tanganyika ya leo, vyeo ambavyo havistahili kabisa kuwepo kwa sababu ya mazingira tuliyomo n.k. n.k.

Katiba yetu ina mapungufu mengi ya wazi na wala hatuhitaji eti kukaa chini tuisome na kuielewa ndipo eti tuanze kudai katiba mpya. Hizo ni hila za wanasiasa walaghai wanaotaka kuturubuni tuamini kwamba eti kwa sababu hatujawahi kuisoma katiba iliyopo basi hatuhitaji katiba mpya.

Nasema tunahitaji katiba mpya si kwa sababu tunaijua vizuri katiba iliyopo. La asha. Tunahitaji katiba mpya kwa sababu tumeona kwamba katiba tuliyo nayo sasa na mfumo mzima wa kisheria unaoongoza nchi hauendani kabisa na mazingira ya kijamii, kisiasa na kiuchumi tuliyo nayo leo.

Usijisumbue kwenda kununua katiba. Tunachohitaji ni iandaliwe rasimu ya Katiba Mpya, tuletewe hiyo rasimu, tuisome, tuijadili, tuichambue na kisha tutoe maoni yetu ili kubadilisha vipengele ambavyo hatukubaliani navyo. Basi.

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.