RSS Feed

Tag Archives: CUF

Hiyo Nakala ya Mswada wa Katiba Mpya inapatika(je) wapi?

Posted on

Jana kulikuwa na Kongamano la Katiba kwenye Ukumbi wa Nkrumah, UDSM. Na, nilivyosoma katika magazeti ya leo, isipokuwa yale ya Chama na Serikali, ni kwamba wadau wengi walionyeshwa kukerwa na mswada utakaopelekwa bungeni mwezi huu ili mchakato wa kuunda katiba mpya uanze. Habari zilizopo zinaonyesha kwamba mswada huo una mapungufu mengi ambayo yanahitaji kurekebishwa kabla ya mswada wenyewe kujadiliwa na hatimaye kuwa sheria.

Na kwa sababu chama-tawala kina idadi kubwa ya wabunge endapo huo mswada utapelekwa hivyo hivyo: Mheshimiwa Cheyo (UDP), Lyatonga Augustine Mrema (TLP), Kafulira (NCCR), wabunge wote wa CUF na wale wa CCM wataupitisha hivyo hivyo na hatimaye itakuwa sheria. Baada ya muda mfupi tutakuja kugundua kwamba tulichotengeneza haikuwa katiba mpya bali tuliiwekea viraka ile ile ya zamani.

Wananchi tungependa kupata nakala ya huo mswada ili nasi tuisome tusipelekwe hivi hivi kiubabe. Nchi ya Tanzania ni yetu sote na si ya watu wachache ambao wako kwenye ngazi za utawala.

Habari ya jana 1: Profesa Safari ajiunga na CHADEMA

Posted on

Nilipozisikia habari za mtu ninayempenda na kumheshimu kama mwanataaluma na mwanafalsafa mzuri kati ya wanazuoni wa Tanzania, Prof. Safari kwamba amejiunga na kambi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akitokea Chama cha Wananchi (CUF) sikushangaa sana.

Kwanza, CUF kwa siku za karibuni wamekosa ile kasi yao na ‘upinzani’ wa kweli. Matamshi ambayo amekuwa akiyatoa mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibarahim Lipumba, yamekuwa yakionyesha dhahiri kwamba CUF ile tuliyoijua imebadilika na sasa imekuwa kama ‘CCM (b)’. Siwezi kuwalaumu sana CUF kwa mabadiliko hayo, nafikiri walikosea pale ambapo walishindwa kubashiri madhara ya muafaka kati yao na Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa upande wa Zanzibar. Wakajikuta kwenye mtego ambao na kuingia na sasa wanalipa gharama. Kwa hiyo kwa mtu yeyote ndani ya CUF ambaye angependa kushindana na siasa za CCM hana jinsi bali kutafuta uwanja mwingine.

Pili, na hii ni kama ushauri kwa uongozi wa CHADEMA. Inawezekana (mimi sina uhakika) aliye-injinia ‘muafaka’ kati ya CCM na CUF ni huyo huyo mliyepokea jana. Kwa hiyo muwe macho nyie CHADEMA isije ikawa ujio wa Safari umeandaliwa makusudi ili kupunguza makali yenu. Msiwe na haraka ya kumpa uongozi hadi hapo mtakapohakikisha kwamba huyo mtu hana ajenda ya siri. Ni tahadhari tu wala sina ‘bifu’ yoyote na profesa.

Neno kutoka kwa rafiki: CUF na CCM ni ndoa. Ndoa bila unyumba yafa

Posted on

Rafiki yangu kwenye facebook alinitumia  meseji hii (by accident):

Pia kumbuka kaka kuwa anayofanya Lipumba ni dalili ya aliyechoka na yuko sokoni kunadi bidhaa mbovu inayotia ukakasi masikio ya wateja.
Cuf kwa kuwananga CHADEMA wakati walishajigamba kuwa wao ni wapinzani inajionyesha wazi kuwa sasa CUF ni CCM B na hakuna shaka juu ya hilo.

Wapenzi wa CUF wakae na kutambua kuwa wao ni sehemu ya CCM kwa kutekeleza sera na mikakati. Maalimu kule Zanzibar anatekeleza ilani ya CCM na Lipumba huku bara anashambulia chama kikuu cha upinzani kama inavyofanya CCM.

Lipumba anasumbuliwa na mchoko wa kisiasa ambao umesha ongeza kasi ya kukidhoofisha chama hicho kwa huku bara. CUF iliyowahi kujitambulisha kama chama ngangari leo hii kimegeuka chama mdebwedo na mlenda kwa kukubali kutumiwa na CCM na wao kujikuta wameingia mtegoni na sasa wao kama wanandoa wanahami unyumba wao usitetereke.

CHADEMA ndio ninao amini kuwa ni wapinzani wa kweli na watetezi waliobeba matumaini ya watanzania.

Vita dhidi ya CHADEMA ina faida gani kwa CUF?

Posted on

CUF tuambieni ajenda yenu

Majuzi gazeti la kila siku hapa nchini lilimnukuu Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, akisema kwamba wanaodhani kwamba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinaweza kushika dola na kuongoza nchi ya Tanzania labda waende kwa “Babu wa Loliondo” wakapate kikombe cha dawa.

Nilipoisoma ile habari kwanza nilishtuka. Sikujua vita ya CUF dhidi ya CHADEMA ni kubwa kiasi hicho. Pia sikutarajia mtu ninayemheshimu sana kama Profesa Lipumba; mtu ambaye kwenye chaguzi zilizopita niliwahi hata kutaka kumpigia kura anaweza kuwa na lugha za kejeli kiasi hicho. Pia sikujua Lipumba amepata wapi ujasiri wa kuongea mambo mazito kama hayo. Kwa jinsi sentensi ilivyokaa ni kama profesa ana uhakika kabisa kwamba CHADEMA haiwezi kuongoza dola. Huo uhakika ameutoa wapi?

Swali nililojiuliza mwishowe lilikuwa: CUF inapata faida gani inapoipiga vita CHADEMA?

Follow

Get every new post delivered to your Inbox.