
CUF tuambieni ajenda yenu
Hivi karibuni ameibuka mtu (mchungaji) na kujitangaza kuwa anatibu (anaponya) magonjwa yote sugu na hata yale ambayo matabibu wamedai hayana tiba. Babu huyu anayeishi maeneo ya Loliondo mkoani Arusha amevitikisa vyombo vya habari vya kitaifa na hata vile vya kimataifa. Kwa ufupi ni kwamba huyu “mponyaji” amejipatia umaarufu wa ghafla. Mambo mengine yamesahaulika kwa muda na mada imekuwa ni “mchungaji wa Loliondo.” Watu kutoka pande mbalimbali za ndani na nje ya nchi wamekuwa wakimiminika kwenda kupewa tiba na babu huyo mwenye fani ya uchungaji.