Watanzania wengi tumekuwa tukitafuta ulaji badala ya kutafuta kutoa mchango kwa maendeleo ya nchi yetu. Utamkuta mtu anakuuliza: “Siku hizi uko wapi?” Unamwambia: “Ninafanya kazi BOT.” Au: “Nipo mamlaka ya mapato Tanzania.” Au wakati mwingine unamweleza: “Ninafanya kazi na ubalozi wa Finland.” Atakachokujibu sasa utashangaa. Mara zote nimekuwa nikisikia watu wakiniambia: “Aisee, huko ndo kwenye pesa. Mambo yako safi sana mzee.” Ukijaribu kuwahoji wanachomaanisha si pesa halali ya mshahara. Bali ni zile pesa waweza kuzipata kama wewe ni mtu wa dili.
Mawazo haya ya dili yatatufikisha wapi?


Ni kawaida kwa binadamu kusahili maisha ili hatimaye aweze kuyaboresha.Hata hivyo, ni vibaya sana kulalama tu bila kuwa na wazo mbadala! akili inayolalama si akili nzuri sana! big up!