Mzee wa Kichagga anarudi CCM?
Magazeti ya hapa Bongo yamekuwa yakiandika habari kuhusu Mhishimiwa mzee wa “Inji Hii”. Mzee yule tuliyesukuma gari lake sana alipokuja Arusha mwaka 1995 ameanza kuwakashfu viongozi wenzake wa vyama vya upinzania na kumtetea JK kwa nguvu zote. Haikuchukui akili za professor kujua kwamba anakoelekea ni kule kule — “baada ya kushauriana na wazee nimeamua kurudi CCM.” Kwa sababu ameshatangaza kwamba hataki tena kugombea Urais 2010 na kutamka hadharani kwamba yeye angependa kugombea ubunge kule Vunjo, ni wazi kwamba anaweza kutimiza malengo yake hayo kwa kugombea kwa tiketi ya CCM.

